Saturday, July 30, 2011

Man U mtalipa kisasi au mta........


 Mabingwa wa Champions League yaani Barcelona, wanayo shuguli nzito kwa kipindi mwisho wa mwezi wa saba na mwezi August barani America.
 Wakiwa bara la Amerika watakutana na timu tatu tofauti moja kati ya timu hizo ni mashetani wekundu yaani Man Utd.
 Ingawa Sir. Alex, kocha wa timu ya Man U bado hajaonyesha imani yake nakikosi chake lakini DeGae amesikika akijitapa na kuisifia timu yake kuwa anaamini itatoka na ushindi mkubwa kwenye mechi hiyo itakayo chezwa tarehe 31 mwezi huu.
 Wadau wa mpira wa miguu duniani akiwemo Pele, wanaufananisha mchezo huu kama vita vya malipizi maana ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 28 mwezi Mei mwaka huu timu hizi zilikutana kwenye fainali za kombe la Champions League.
 Matokeo ya fainali ile yaliiacha dunia nzima ya mpira wa miguu midomo wazi baada ya Man U kupokea kichapo cha magoli 3-0, mmoja kati ya wakali walioiumiza Man U wengine hupenda kumuita DOKTA yaani Messi hatokuwepo kwenye kikosi cha Barca baada ya kuwa yupo kwenye likizo kwao Argentina.
 Barca watakuwa wakicheza 4-3-3, akiwemo Valles, Abidal, Pique, Puyol, Fontas, Thiago, Benquet, Iniesta, Afellay, Jonathan bila kumsahau Villa.
 Pia Man U itasukuma mtanange huu ikiwa inacheza 4-3-3, ikimchezesha De Gae, Vidic, Ferdinand, Evra, Young, Carrick,  Anderson, Park,Berbatov, Rooney.
 Barcelona pia wakiwa bado bara la Amerika watachuana na CD Gadalajara mnamo tarehe 3 August na Club America mnamo tarehe 6 August.
 Usiku wa kuamkia leo nahisi jiji letu litakuwa na shamsham sana, yaani tukimaliza tu shngwe za fiesta 2011, usiku mzito tutakuwa tanapagawa na mechi hii kati ya Man U na Barca pale Washington DC.
                                                                                                      Masekepa Asangama

Luda ana zaidi ya show na swagg "TUJIFUNZE"


 Mshkaji anaitwa Christopher Brian Bridges kwa jina kamili, nimejiuliza hii aka ya Ludcriss ilikujaje nakosa jibu sahii, maana haifanani kabisa na jina lake halisi....
 Jamaa alizaliwa mwaka 1977, Sep 11 pale Champaign nchini U.S.A...
 Alianza mziki 1998 na leo ana album saba na leo atakuwa na bonge moja la concert hapa jijini kwenye viwanja vya Leaders Club.
 Najua marafiki wengi tutakuwa pale usiku huu, ila kama rafiki nimewaokotea kastory nataka kushare na nyinyi kumhusu Luda.
 Kama nlivyokwisha sema kuwa hii ni album ya saba ya msanii huyu, inaitwa "Battle of sexes" ambayo aliiachia tarehe 9, march mwaka huu.
 Idea ya album hii ilikuwa kuwakutanisha Luda na mmoja kati ya wasanii walio chini ya lebo yake iitwayo "disturbing the peace au DTP". Yani kama unavyoona Lil'wayne alivyokuwa na Nicki Minaj kwenye album yao mpya.
 Mapema kabla ya kumaliza kurekodi album hiyo ambayo kabla yakupewa jina la battle of sexes ilipewa jina la back to back, mwanadada huyo kwa jina la Shawnna alivunja mkataba na lebo ya Luda na kuhamia kwenye lebo ya T-Pain iitwayo Nappy boy Ent.
 Kuhama kwa mwanadada huyo kulivuruga sana ratiba za Ludacriss na kupelekea kuanza upya kurekodi album hiyo na kuiita Batte of sexes.
 Licha ya tatizo hilo Luda alifanikiwa kumaliza kurekodi album hiyo na tarehe 8 Dec 2009 alichia ngoma ya kwanza kutoka kwenye album hiyo na nyimbo hiyo "how low" ilifanya vizuri na mwanzo wa mwaka huu aliachia album na ilifika mauzo ya Gold baada ya kuuza nakala 137000 kwa wiki ya kwanza sokoni.
 Swala linakuja Je! Ingekuwa ni msanii wa bongo falva kakutwa na matatizo kama hayo angemaliza kurekodi hiyo album kweli?
 Hakika HAPANA, zaidi wangeishia kulumabana kwenye vituo vya habari na kutupiana maneno tu mwisho kuharibu heshima zao na vipaji vyao pia,
                                                                                                            Africa Nyumbani.

Friday, July 29, 2011

Tusiharibu mimba, watoto ni faraja kubwa.....

 Jina langu ni "baba wawili", ni kijana wa kawaida kabisa na ili kuthibitisha ukawaida wangu jamani hata kazi maalum sina, ila hilo sio tatizo sana kwangu.
 Ishu ni hawa madogo wawili "mapacha" wangu, ambao niliwapata nikiwa mdogo sana.... Na hiyo ndio sababu leo timu ya bloglab imetoa nafasi hii kwangu ili niwe naandika kuhusu maisha yangu na watoto wangu ili kijana yeyote atakaye soma simulizi hizi apate nguvu kimaisha kuhusu familia na hatma yake namba ya vijana wanaotoa mimba kila siku na hata wanaopoteza maisha kupungua kabisa.
 Kama nlivyokwisha kusema kuwa niliwapata hawa mapacha nikiwa mdogo sana, na mara nyingi vijana kama mimi ambao wanakuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mara tu linapotokea swala la mimba mahusiano hulegalega sana.
 Sawa hata mimi siwezi kukataa hata mara moja kuwa siku ile mama wawili aliponiambia kuwa anahisi ana ujauzito sikupata mshtuko, HAPANA! Nilipata mshtuko tena mkubwa sana, nakumbuka tulikuwa nyumbani kwangu, hata hamu ya kuendelea kupumzika iliisha na niliamua kuondoka zangu na kumwacha mpenzi wangu chumbani peke yake.
 Sawa sababu ni nyingi sana ambazo humpelekea kijana kupatwa mshtuko na hatma yake kuamua maamuzi hasi ili kuondokana na jambo hilo kabisa, wengine hukimbia mpaka miji ili kuepuka tatizo, wengine hukataa kabisa kuwa hawahusiki na ujauzito huo na wengine huthubutu kufanya "abortion" yaani kuitoa mimba.
 Ila nisingependa kuwa mwalimu kwa kiasi kikubwa bali kusimulia tu maisha yangu na wanangu hawa, ndani ya simulizi hizi pia kijana utapata mambo meengi mazuri na hii itakujenga hata siku utakapo kuwa na hali kama yangu iwe rahisi kuendanna na hali hiyo.
 Doto anaitwa "Dido" na kulwa "Obama", nawapenda sana..... Mara nyingine natamani wawe marafiki zangu na kuutoa huu ubaba kabisa labda wangenipenda zaidi na kuniamini bila kuwapo chembe ya uoga kuwa mi ni baba ntawachapa au ntawakasirikia...
 Naamini sio rahisi ila sitochoka kuwajengea imani hiyo ndo maana hata ukija nyumbani siku moja utasikia wananiita "kaka", na naamini ipo siku wataniita rafiki pia.
 Wameleta faraja kubwa kwenye familia yangu, faraja ambayo mimi na mama yao hatukuwa nayo kabla... Sasa ndani ni furaha tu, Dido atacheza hivi Obama vile basi ni furaha tupu jamani....
 Nakaaga na kuwaza je mimi na mama yake tungeamua kuitoa mimba, watoto hawa wangekuwa wapi leo.... Je! Furaha hii tungeipata wapi tena, hakika tusingeipata popote. Basi kumbe ulikuwa uamuzi wa busara sana kutokuikana mimba.
 Ingawa ulikuwa uamuzi mzito sana, kwani sikuwa na kazi, mama pia hakuwa na kazi.... Wapi tungepata pesa za kuwalisha watoto hawa? Kila jibu lililokuja wakati hule lilikuwa tatizo. Lakini tulipiga moyo konde na kuamua kuilea.
 Haya leo ngoja niishie hapa.... Ila jamani vijana wenzangu "mimba" msizitupe...... Mtoto huwa neema kubwa jamani, natamani mngeniona na furaha yangu leo.
                                                                                                         Tukutane wiki ijayo
                                                                                                                   Baba Wawili

Nicki Minaj na Roman Zolanski ni TWINS!!!!



 Licha ya umaarufu alionao Nicki Minaj, vituko na habari tofauti kumuhusu zinazaliwa kila kukicha.
 Hivi karibuni ametoa kali baada ya kumtambulisha dada yake ambaye ni pacha wake, Nicki Minaj akiwa kwenye moja ya mahojiano kwenye kituo maarufu cha matangazo kijulikanacho kama VIBE, alinukuliwa akisema "the one you see in buttoms up song with Trey, thats not Nicki Minaj, instead she is Roman Zolanski".
 Ina maana muda wote ulimwengu ukidhani kuwa yule ni Minaj, yeye mwenyewe alikana na kusema yule si yeye ni pacha wake Roman Zolanski.
 Pia alitanabaisha kuwa mama yao anasikika kwenye remix ya nyimbo ya romans revenge akirap sehemu ndogo kwa lafudhi ya kiingereza cha ya uingereza.
 Zaidi Minaj alisema "Roman was born inside me, i become her when i get ungry, she is a demon inside me".... Pia wanaharakati wa hip pop wamemfananisha Roman na Slim shady ambaye nayeye ni demon wa Eminems.
 Ndio sababu remix ya nyimbo ya Romans revenge, mwanadada Minaj aliamua kuwakutanisha wakali hawa yaani Roman Zolanski na Slim shady.
 Swala ni kwamba je kwa hapa TZ wapo wasanii wanaowajua ndugu zao kwa maana ya mizuka yao, na kuwatumia vizuri.... Au ni bangi tu mwanzo mwisho?
                                                                                           Baadae rafiki zangu,
                                                                                                                    Ian.

Saturday, July 23, 2011

Aibu, saa saa simusimu jaman...

 Siku moja nilikuwa kwenye daladala, natoka zangu chuoni naelekea hostel. Ndani ya lili gari kuna mmoja kati ya masuperstar wetu wa bongo jina naomba nilihifadhi.
 Nikamuuliza “samahani kaka, sasa  hivi ni saa ngapi?”. Jibu alilonipa mmmhh nikamvua vyeo vyote jamani….. uanjua alinijibu nini!!!!!
 Eti “ooh sorry, simu yangu haina charge dadangu, siunajua mambo ya mgao wa umeme” hahahahahahha, jamani siku njema na hao mastar wenu…..
                                                                                                                  Sara Sean

Jamani Gucci Mane sio mmiliki wa kampuni ya GUCCI....


 Saba kati ya wajanja kumi wa mtaa wanaamini kuwa Gucci Mane msanii wa hip pop nchini marekani ndiye mmiliki wa GUCCI kampuni ya mavazi kama ilivyo kwa Sean Combs aka P.Diddy na kampuni yake ya SEAN JOHNS.
 Siajabu hata wewe piw ni mmoja kati ya hao wanaoamini hivyo ila ukweli ni kwamba Gucci mane na GUCCI ni mambo mawili tofauti kabisa.
 Ili kukuweka sawa kuhusu hili leo ntakupa ukweli kuhusu GUCCI, kwanza kabisa mmiliki wa kwanza au mwa nzilishi wa kampuni ya GUCCI ni Guccio Gucci mzawa wa Florence Italy.
 Kabla ya kuanzisha kampuni hiyo Guccio alikuwa mfanyakazi katika baadhi ya mahoteli makubwa sana mjini Paris na London pia, akiwa huko bwana Guccio alipenda sana uzuri wa mabegi yalikuwa yanaingia na wageni toka nchi mbalimbali.
 Aliporudi kwao Italy  akaamua kufungua duka dogo amblo waliuza viyu kama mabegi, viatu, wallets, set cover za magari n.k. Hapo ndipo mwanzo wa kampuni ya GUCCI.
 Baadae akishirikiana na wanawe watatu wakiume yaani Aldo, Vasco na Rodolfo waliweza kufungua maduka zaidi kwenye miji mashuhuri duniani  mfano Milan, Rome na baadae New York Marekani.
 Ingawa pametoke kampuni nyingi za mavazi duniani bado GUCCI imekuwa juu sana, na mpaka sasa ina zaidi ya maduka 237 dunia nzima.
 So kwa habari hiyo kwa ufupi naamini tumefunguka sana kuhusu hivi vitu.
 Wengi wetu kiukweli licha ya kuwa mashbiki wa msanii lil`wayne hatujui ukweli kumhsu baba yake mzazi. Hali hii imekuwa hivi kutokana na baadhi ya rafiki kudhani kuwa baba mzazi wa lil`wayne ni Bird Man.
 Ukweli ni kwamba baba mzazi wa star huyu wa hip pop ni Dwayne Michael Carter, ambaye alifariki wakati lil`wayne alipokuwa mdogo sana.
 Lil Wayne pia alipewa jina hilohilo la Dwayne, lakini kwasababu hakupata kabisa malezi ya baba aliamua kuitoa D na kubakisha wayne tu… na mpaka leo anatumia jina hilo.
 Kali zaidi kuhusu wayne ni kwamba alipata motto wake wa kwanza akiwa na umri wa miaka 15…… duh hii ni balaaa, kumbe mpaka ulaya watoto huzaa watoto.
                                                                                                         Nice times rafiki